IQNA

Wanachuo wa Iran wataka Sheikh Zakzaky aachiwe huru

Umati mkubwa wa wanachuo wa Kiirani na wa kigeni pamoja na wananchi Jumatano 17 Julai walikusanyika mbele ya ubalozi wa Nigeria hapa mjini Tehran kuonyesha mshikamano na uungaji mkono wao kwa kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria, Sheikh Ibrahim Zakzaky.