IQNA

Msikiti wa Jamia Glasgow ni kituo cha kudunga chanjo ya COVID-19

20:49 - December 28, 2021
Habari ID: 3474736
TEHRAN (IQNA)- Msikiti wa Jamia mjini Glasgow, Scotland sasa ni kituo cha kuwadunga watu dozi ya tatu ya chanjo ya COVID-19.

Queues outside a vaccine centre in Glasgow this week. Centres have experienced a rush of people booking their booster jabs

Kituo cha chanjo ndani ya msikiti huo kimefunguliwa Jumatatu ambapo wakuu wa Huduma ya Kitaifa ya Afya Uingereza (NHS) Ukanda wa Glasgow na Clyde (NHSGGC) wametangaza kupitia Twitter kuwa kutakuwa na wahudumu 45 wa kudunga chanjo katika kituo hicho.

Maafisa wa afya katika eneo la (NHSGGC) wametoa wito kwa wananchi kufika msikitini hapo kupata chanjo kwani kumeshuhudiwa ongezeko la maambukizi ya COVID-19 na hospitali zinakaribia kujaa.

Hayo yanajiri wakati ambao Jumatatu  27 Disemba 2021 watu 98,515 waliambukizwa COVID-19 kote nchini Uingereza ambapo jumla ya maambukizi nchini humo sasa ni milioni 12. Aidha Jumatatu watu 143 walipoteza maisha kutoana na COVID-19 na kufanya idadi ya walipoteza maisha kupindukia 98,515 hadi sasa.

3477122

captcha