IQNA – Mji wa kihistoria wa Isfahan, katikati ya Iran, uliamka Ijumaa, tarehe 19 Disemba 2025, ukishuhudia mandhari ya kuvutia pale theluji ya kwanza ya vuli ilipolala juu ya mandhari zake maarufu.
Upepo wa theluji laini ulienea katika mji huo ambao ni maarufu Kiajemi kama Nisfe Jehan yaani “Nusu ya Dunia." Neema hiyo ya mmwenyezi Mungu ilieneza furaha na kuleta bashasha halisi mitaani.