IQNA

Tamasha Kuu la Chakula Cha Halal Limepangwa Kufanyika katika Uwanja wa London

11:24 - September 09, 2023
Habari ID: 3477571
LONDON (IQNA) - Uwanja wa London unatazamiwa kuandaa Tamasha la Kila mwaka la Chakula cha Halali cha Dunia mwezi huu.

Tukio hilo kuu linatazamiwa kufanyika mwezi  Septemba  tarehe 23-24 huku mratibu wake Waleed Jahangir akielezea kufurahishwa na kurejea kwenye ukumbi huo wa kipekee.

 

Tunafuraha kurejea kwenye Uwanja wa michezo wa London, katikati mwa jumuiya, kwa ajili ya tukio kubwa zaidi la chakula cha halal duniani, alisema Waleed Jahangir, Mkurugenzi Mkuu wa Tamasha za Algebra, British Muslim Magazine ilitoa ripoti.

Tamasha la Chakula Halali Ulimwenguni ni fursa kwa wanajamii wote kukusanyika pamoja na kupata ladha za ulimwengu chini ya paa moja na familia na marafiki.

Tamasha hilo, ambalo zamani liliitwa Tamasha la Chakula la Halali la Landan, limefanyika kwa miaka minane na litaangazia maduka 200 ya vyakula vya halali.

Mkurugenzi Mtendaji wa London Stadium Graham Gilmore alikaribisha tamasha hilo kwa mwaka wake wa tatu. Tunafurahi kukaribisha tena tamasha hili la ajabu la chakula kwa mwaka wake wa tatu katika Uwanja wa London Stadium  alisema.

Eneo letu linafaa kwa sherehe hii, ambayo inaleta pamoja chakula, muziki, na utamaduni wa jamii ya Waislamu kwa wote kufurahia katikati mwa Landan Mashariki.

Ushiriki wa Ajabu Humhimiza Mratibu Kuzingatia Tamasha la Halali la Siku 3, nchini Uingereza

Washirika wa tamasha hilo ni pamoja na Polisi wa Metropolitan wa Landan, Jumuiya ya Biashara ya Kiislamu ya Uingereza, Tariq Halal Meats, na Jarida la Waislamu wa Uingereza.

Tamasha la Chakula la Halali la Landan kwa kawaida huvutia umati mkubwa wa wapenda chakula kila mwezi wa Septemba.

Nini maana ya chakula cha Halali?

Chakula cha Halali kinarejelea chakula kinachofuata miongozo ya lishe iliyowekwa kwenye Qur’ani Tukufu na Hadith, ambazo ni maandishi ya kidini ya Uislamu, Ina mahitaji mawili muhimu Kwanza, chakula lazima kitoke kwenye chanzo halali na kinachoruhusiwa, Hii ina maana kwamba baadhi ya vitu, kama vile nyama ya nguruwe, damu, pombe, na wanyama waliokufa kwa kawaida au hawakuchinjwa kwa usahihi, ni haramu kwa Waislamu, Pili, mchakato wa kuandaa, usindikaji, na kuhifadhi chakula lazima ufanyike kwa njia safi na isiyo na uchafu, Kwa mfano, vifaa vinavyotumiwa kuchinja wanyama lazima viwe safi na vyenye ncha kali, na wanyama lazima wauawe haraka na kwa njia maalum.

Chakula cha Halali sio tu wajibu wa kidini kwa Waislamu, lakini pia huwakikisha usafi, ubora, na usalama wa chakula Zaidi ya hayo, ina mazingira, ustawi wa wanyama, na manufaa ya afya.

 

3485081

Kishikizo: chakula halali usalama
captcha